Habari

Mario Van Peebles kuzindua filamu yake Mlimani City


Wakazi wa Dar es Salaam watanufaika na ujio wa muigizaji na muongozaji wa filamu wa Hollywood Mario Van Peebles aliyealikwa mwaka huu kama mgeni wa heshima kwenye tamasha la filamu la kimataifa Zanzibar, ZIFF.
Van Peebles ataizindua filamu yake ya mwaka huu iitwayo ‘We The Party’ ambayo ameiongoza na kuigiza pia.
Kwa ushirikiano na ZIFF, kutafanyika ‘red carpet premier’ ya filamu ya ‘We the Party’ kwenye ukumbi wa Century Cinemax cinema wa Mlimani City.
Tukio hilo litahudhuriwa na yeye mwenyewe Mario Van Peebles na mwanae wa kiume Mandela Van Peebles aliyeigiza kama mhusika mkuu kwenye filamu hiyo.
Filamu hiyo itaoneshwa kwa siku tano mfululizo ili kutoa muda zaidi kwa watu kuiona.
We The Party iliyoigizwa jijini Los Angeles inahusisha marafiki watano wanafunzi wa high school wanaozungukwa na mapenzi, pesa, kujirusha, chuo, sex, bullies, Facebook na mambo mengine.
Rapper Snoop Dogg anaye ameigiza kwenye filamu hiyo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents