Burudani

Mapenzi ndani ya Big Brother yajenga uadui ‘mkali’ kati ya Kenya na Nigeria.


Jana wapenzi katika jumba la Big Brother Africa, Prezzo na Goldie wamezinguana tena baada ya Prezzo kumwambia Goldie, “you are a quitter, you are a runner, run away like you always do.” Pia alimwambia kuwa hakukuwa na haja Goldie kumwokoa na eviction.
Ugomvi huo wa Prezzo kutoka Kenya na Goldie kutoka Nigeria umenunuliwa na wananchi wa Kenya na wale wa Nigeria. Vita vya maneno na matusi vimetawala ukurasa maalumu wa Big Brother Africa wenye ‘fans’ 859,622 mpaka sasa.
Wakenya na wanaijeria wamejikuta katika vita nzito ya maneno kiasi cha kuhatarisha uhusiano kati ya nchi hizo mbili.
Kenya, I don’t remember u winning BB, by the look of things u r not going to win not anytime soon… Sit ur asses down for a minute and watch the game, always insulting that’s what u knw best. Last time u were busy with SA now is Nigeria?” aliandika Nonhlanhla Sambo.
Grace Wanjiku wa Kenya aliandika, “si wakenya mwajua we are a working nation! Hawa waoga na sa hawana kazi,they eat /sleep bba!24/7 nendeni mkachape kazi.”
Mkenya mmoja aitwaye John Kisindai Kulundu aliamua kuziponda filamu za wanaijeria kwa kusema, “Only retarded villagers watch those predictable naija movies.lol.”
Kulundu hakukomea hapo, aliwaangushia wanaijeria bomu jingine, “nigerians have invaded africans cities because of insecurity and poverty in there country,we shall kick u back 2 die in your country,kaa mbali na sisi msituambukize ujinga.”
Kitendo cha wakenya kuchanganya Kiswahili kwenye comments zao zilimkera Mary Esosuota aliyesema, “Only cowards murmur so dey wont be heard…anyone bold enough shud write boldly and air their views for others to understand.”
Wanaijeria hawakukubali kushindwa, Maureen Eboh alitupa bomu kwa wakenya, “What a shame kenyans, c as dem dey wash una wif soda soap nd water, chai c poverty, not even detegent soap buh soda, una own don finish b dat oh.”
Mnaijeria mwingine Tunde Olawole aliandika, “Foolish kenyans they are all affected by meningitis which is a mentor to their mental image u will alwayz be our wast.teamnaija.”

Kama desturi ya watanzania wasiopenda makuu, mtanzania Koli Collins hakupendezwa na vita hiyo ya maneno kati ya wanaijeria na wakenya kwa kuwaambia, “Wakenya nawaomba,acheni matusi ili tusiwakwaze watu wa nchi zingine,tusije tukachimbia Prezzo kaburi kama vile watu wa Afrika kusini walivyomchimbia bibi kizee wao almaarufu barbs….sababu ya kujigamba na matusi,tusome funzo kutoka kwao, Proudly Tanzanian.”
Unadhani vita hii ya maneno kati ya wanaijeria na wakenya kutokana na Big Brother inaweza kuleta uadui kati ya nchi hizo baadaye?

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents