Burudani
Manecky: Muziki unaotengezwa Tanzania umeshiba
Producer wa AM Records, Manecky amesema kuna maendeleo makubwa kwenye muziki wa Tanzania katika upande wa production.
Manecky ambaye aliwahi kushinda tuzo ya mtayarishaji bora wa muziki 2013 katika tuzo za KTMA. ameiambia Bongo5 kuwa watayarishaji wa Bongo wamejifunza vingi kutoka kwa wenzao wa nje hali iliyosabisha muziki wa Tanzania uendeleee kupasua mawimbi kimataifa.
“Kwa mwaka huu muziki wetu umezidi kuwa mkubwa kwa sababu kila muda unavyozidi kwenda ma-producer kuna vitu tunaviongeza kwenye muziki wetu,” amesema. “Mengi tunajifunza kutokana na watu wa nje inafanya tuweze kubadilisha vya kwetu na kuboresha zaidi. Kwa upande wa production, production zimezidi kuwa nzuri pia muziki wetu pia umebadilika,” aliongeza.