Michezo
Mahakama kuu ya China imempa ushindi huu Michael Jordan
Mchezaji wa zamani wa mpira wa Kikapu Michael Jordan, ambaye alifungua kesi ambayo alikuwa anaishitaki kampuni ya kichina iliyokuwa inatumia jina lake kujiingizia kipato. Mahakama kuu ya China imempa ushindi katika kesi hiyo.
Michael Jordan tangu mwaka 2012 alianza malalamiko dhidi ya Kampuni ya Qiaodan Sports.
Ampapo kampuni hiyo ilikuwa ikitumia jina lake kuuza bidhaa zenye jina la Jordan lakini kwa kichina “Chee-ow-dahn.” Mchezaji huyu amesema amefurahi kuona jina lake linaheshimiwa.
Mahakama imewaambia wachina wasitumie hilo jina la Jordan kwa kichina lakini wamewaachia mwanya kuwa wanaweza kuandika jina hilo kwa herufi za kirumi Qiaodan”Chee-ow-dahn.”