Burudani

Mahaba ya mpenzi wangu yamenisukuma kuandika wimbo Sijiwezi – Nay wa Mitego

Msanii wa muziki wa hip hip Nay wa Mitego amedai hawezi kuandika wimbo wa mapenzi kama hana filling ya mapenzi au hayupo kwenye mahusiano.

Akiongea na Bongo5 Jumatatu hii, Nay amedai wimbo wake mpya ‘Sijiwezi’ ameuandika kutokana na kupewa mahaba mazito kutoka kwa mpenzi wake.

“Mimi siwezi kuandika wimbo wa mapenzi bila kupata filling ya mpenzi kutoka kwa mpenzi wangu au watu wangu wa karibu ndio maana hata unaona na nyimbo chache sana za mapenzi,” alisema Nay. “Hata Sijiwezi umetokana na maisha yangu ya ndani na mpenzi wangu. Nikaona hapa kuna sababu ya kuandika kitu na kweli nimefanya na namshukuru Mungu ngoma inaenda,”

Rapa huyo anawashukuru mashabiki wa muziki wake kwa kuupokea vizuri wimbo huo katika kipindi cha muda mfupi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents