Madonna aachia nyimbo sita kwa mpigo kama zawadi ya X-mas baada ya album yake kuvuja
Madonna amewapa mashabiki wake zawadi ya sikukuu kwa kuachia nyimbo sita zinazotoka kwenye album yake mpya.
Lakini sio tu kwamba ameamua kwa mapenzi yake kuachia kiasi hicho kikubwa cha nyimbo kwa mara moja, bali ni kufuatia album yake iitwayo “Rebel Heart” kuvuja na kulazimika kufanya hivyo.
“Nilikuwa natarajia kuachia single mpya ‘Living for Love’ kwenye Valentine’s day pamoja na album ingefuatia…” alisema Madonna. “Ningependa mashabiki wangu kusikiliza baadhi ya nyimbo zilizokamilika badala ya vipande vya nyimbo zilizosambaa. Naomba mchukue hizi nyimbo sita kama zawadi ya mapema ya Christmas.”
Nyimbo alizoachia Madonna ni “B*tch I’m Madonna” aliomshirikisha Nicki Minaj, “Living for Love”, “Devil Pray”, “Ghosttown”, “Unapologetic B*tch”, pamoja na “Illuminati”.