Burudani

Madee adai ‘Sio Mimi’ (Pombe Yangu) imeshamuingizia shilingi milioni 130 hadi sasa

Hit maker wa Sio Mimi aka Pombe yangu, Madee amesema hadi sasa ameshaingiza zaidi ya shilingi milioni 130 kutokana na show mbalimbali alizopata hivi karibuni tangu aachie wimbo wa huo.

Kulia ni Madee ,akiwa na Abdul Kiba Serengeti fiesta 2013 Tabora.
Kulia ni Madee ,akiwa na Abdul Kiba Serengeti fiesta 2013 Tabora.

Madee amesema pamoja na show za kawaida, makampuni ya simu yameshamsainisha show zaidi ya 12 ambazo zimekuwa zikimpa mkwanja wa nguvu.

Akiongea na Bongo5, Madee ambaye atatumbuiza kwenye show ya Serengeti Fiesta 2013 mjini Singida leo, amesema pia muziki wake umetoa fursa kwa vijana wa Tip Top Connection ambao amekuwa akifanya nao kazi katika show mbalimbali.

“Nimekua nikiingiza Milioni 2 hadi 3 kwa wiki kutokana na Pombe Yangu. Ni tofauti na awali wakati tunaanza muziki kwa sasa ukifanya wimbo ukawa mkali basi ujue pesa zipo zinakusubiri. Pamoja na hayo wimbo ya Pombe Yangu umetoa fursa kwa vijana ambao nakuwanao kwenye show zang. Filamu ya “Pombe Yangu” pia imeajiri vijana,watu wametengeneza T-Shirt ‘Nani kamwaga Pombe Yangu’. Hyo ni fursa wameitumia kupitia Pombe Yangu, alisema Madee.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents