Burudani
Madee akabidhiwa rasmi mtoto wake wa kike aishi naye
Rais wa Manzese, Madee amekabidhiwa rasmi mwanae wa kike kuishi naye.
Madee akiwa amemfuata mtoto wake shule
Akizungumzana Bongo5 leo, Madee alisema mtoto huyo alikaa kwa mama yake kwakuwa umri wa kukabidhiwa ulikuwa haujafika.
“Unajua yule ni mtoto wangu na sikuwa nae kwa sababu alikuwa hajafika umri wa kukadhiwa ili niweze kukaa naye. Na sheria yetu inasema mpaka miaka 8, mama yake anakaa kwake na mimi nakaa kwangu.
Kwahiyo muda mwingi sana alikuwa na mama yake ila baada ya kutimiza umri kukabidhiwa na kuweza kukaa naye ndo umefika. Sasa hivi nipo naye, nafurahi sana.”