Habari

Madaktari wa Kenya wamaliza mgomo wa siku 100 baada na kuafikiana serikali yao

Serikali ya Kenya pamoja na madaktari nchini humo, hatimaye wametia sahihi makubaliano ya kurudi kazini.

Hii ni baada ya mgomo wa madaktari nchini kenya, ambao umedumu siku mia moja na kuathiri vibaya huduma za afya nchini humo.

Chama cha madaktari kikiongozwa na mwenyekiri wake Oroko Samuel, kuliungana na waziri wa Afya Cleopha Mailu kwenye ofisi za magavana wakati wa kutiwa sahihi makubaliano hayo.

Awali kulikuwa na hofu wakati madaktari walikataa kuingia ofisi ambapo makubaliano hayo yangetiwa sahihi, wakilalamikia utata wa vipengee fulani.

Madaktari walianza mgomo huo wakidai kuwa serikali imeshindwa kutimiza makubaliano waliyoafikiana, ya nyongeza ya mishahara yao na kuboreshwa kwa mazingira ya kufanya kazi.

Wiki iliyopita rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, alitangaza kuwa madaktari wangechukuliwa hatua iwapo hawangemaliza mgomo wao.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents