Burudani

Macklemore aeleza kuumizwa baada ya kusitishwa kwa tamasha la TribeOne, Afrika Kusini

Rapper wa Marekani, Macklemore ametumia mtandao wa Facebook kueleza kusikitishwa kwake kutokana na kusitishwa kwa tamasha la TribeOne lililokuwa lifanyike wiki ijayo nchini Afrika Kusini.

macklemore-boston-rappers

Waandaji wa tamasha hilo la siku tatu, Alhamis hii walitangaza kusitishwa kwake kwa madai kuwa maandalizi yake yamechelewa na hivyo wasingeweza kufanya tamasha walilokuwa wamedhamiria. Tamasha hilo lilitarajiwa kuwa kubwa zaidi kuwahi kufanyika barani Afrika ambapo Nicki Minaj na J Cole wangetumbuiza pia.

Kutokana na habari hiyo, Macklemore ameandika: South Africa.. We are super bummed about the Tribe One Festival being canceled. We were really looking forward to this show and hope to have the opportunity to perform for you soon!”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents