Burudani
Lupita Nyong’o kuigiza kwenye filamu mpya ‘Queen of Katwe’ itakayofanyika Uganda
Mshindi wa Oscar Lupita Nyong’o anatarajiwa kushiriki kushoot filamu mpya iitwayo ‘ Queen of Katwe’ ambayo atakuwa muigizaji mkuu.
Kwa mujibu wa mtandao wa Uganda, ‘Queen of Katwe’ inatarajiwa kushootiwa nchini humo ikiongozwa na director aitwaye Mira Nair.
Filamu hiyo itabeba hadithi inayotokana na kitabu cha Tim Crothers kiitwacho ‘The Queen of Katwe: A Story of Life, Chess, and One Extraordinary Girl’s Dream of Becoming a Grandmaster’
Katwe ni eneo linalopatikana katika jiji la Kampala nchini Uganda.