BurudaniMitindo

Lundenga ajibu swali la kama Sitti Mtemvu atanyang’anywa zawadi alizopewa aliposhinda taji la Miss Tanzania 2014

Mkurugenzi wa LINO International Agency ambao ni waandaaji wa mashindano ya Miss Tanzania, Hashim Lundenga amesema miongoni mwa maswali aliyokutana nayo kwa wingi jana kwenye ‘Kikaangoni’ ya EATV, ni pamoja na swala la Sitti Mtemvu kama atanyang’anywa zawadi alizopewa ili akabidhiwe aliyevishwa taji hilo baada ya yeye kujivua.

Sitti na Lundenga

“Kwanza hii ni mara ya kwanza kwa Tanzania mtu kujivua taji, na kwenye kanuni zetu haikuelezwa wazi wazi kwamba mtu akivua taji tunachukua zawadi tunamkabidhi mtu mwingine ama hivyo,” Lundenga ameiambia E-Newz ya EATV.

Lundenga amesema kuwa Sitti hatanyang’anywa zawadi kwasababu hakuvuliwa taji bali alijivua mwenyewe.

“lakini bado tuna majadiliano na wadau wetu masponsors tuangalie namna ya kufanya, kama kuna zawadi zimebaki atapewa lakini zawadi ambazo amepewa nafikiri hataweza kurudisha kwasababu hakuvuliwa, kama tungemvua kwa makosa angeweza kurudisha lakini hatujamvua kajivua mwenyewe”.

Zawadi iliyotolewa mwaka huu kwa mshindi wa Miss Tanzania 2014 ni shilingi milioni 18.

Related Articles

Leave a Reply

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents