Habari

Lord Eyez kesho kuzungumza na waandishi wa habari

Msanii Lord Eyez

Rapper wa kundi la Nako 2 Nako Soldiers na Weusi, Lord Eyez, kesho anatarajia kuzungumza na waandishi wa habari kuelezea shutuma dhidi yake za kudaiwa kushiriki kuiba vifaa vya gari vya Ommy Dimpoz.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na rapper wa Arusha ambaye pia ni member wa Weusi, Nikki wa Pili, Lord Eyez atakuwa na mwanasheria wake.

Amesema mkutano huo na waandishi wa habari utafanyika katika hoteli iliyopo jirani na Mlimani City, jijini Dar es Salaam.

Lord Eyez yuko nje kwa dhamana na anakabiliwa na makosa zaidi ya 30 katika kesi hiyo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents