Habari

Lissu, kamanda wa polisi Ilala ‘wachuana’ kortini

Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na kamanda wa polisi wa Mkoa wa Ilala, Salum Hamdani wamechuana mahakamani katika kesi ya uchochezi inayomkabili mbunge huyo na wahariri wa gazeti la Mawio.

Hata hivyo, Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba leo atatoa uamuzi wa kama Hamdani aeleze anachokifahamu juu ya Katiba ya Zanzibar na kama Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha anaweza kufuta matokeo ya uchaguzi.

Hiyo ilikuwa ni baada ya Lissu kumtaka Hamdani, ambaye ni shahidi wa upande wa mashtaka, aeleze anachokifahamu kuhusu Katiba ya Zanzibar na kama Jecha anaweza kufuta matokeo ya uchaguzi.

Hakimu Simba alifikia uamuzi huo baada ya wakili wa Serikali, Paul Kadushi kupinga shahidi huyo kujibu swali hilo kwa sababu si mtaalamu wa sheria wala katiba hivyo hawezi kutoa tafsiri ya Katiba ya Zanzibar na kwamba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza masuala ya kikatiba.

Lissu alimhoji Hamdani maelezo yake yaliyo polisi aliyaandika kama nani? Mahojiano yao yalikuwa kama ifuatavyo:

Hamdani: Niliandika maelezo yangu kama mlalamikaji na kwamba mikusanyiko hiyo haikuwa haramu, ilikuwa halali kisheria.

Lissu: Mweleze mheshimiwa kama mihemko kisheria inakatazwa ama la?

Hamdani: Haikatazwi.

By: Emmy Mwaipopo

Chanzo: Mwananchi

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents