Burudani
Lionel Richie akanusha uvumi kuwa yeye ni baba mzazi wa Khloe Kardashian
Mwimbaji mkongwe Lionel Richie amekanusha uvumi uliosambaa kuwa yeye ni baba mzazi wa dada yake na Kim Kardashian aitwaye Khloe Kardashian.
Mwanzoni mwa mwezi huu chanzo kimoja ambacho kilidai kuwa karibu na Lionel, kiliiambia In Touch kuwa mama yao Kim K, Kriss Jenner aliwahi kuwa na uhusiano na Lionel Richie miaka ya 1980 na Khloe Kardashian ni zao la uhusiano wao.
Khloe Kardashian
Baada ya Lionel kuulizwa na TMZ Jumatatu usiku wiki hii kama ni kweli yeye ndiye baba mzazi wa Khloe alijibu, “No of course not,” na akaendelea kwa kusema “But you know what, they are my kids, they grew up in my house.”