Burudani
Lifahamu jibu la Wakazi kama muziki unamlipa
Rapper Wakazi amedai kuwa ameanza kuona matunda ya muziki anaoufanya.
Akizungumza jana kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio wakati akitambulisha wimbo yake mpya PMD, Wakazi alisema kwa sasa anaishi kutokana na matunda ya muziki wake.
“Show pamoja na kuuza nyimbo,” alisema. “Sasa hivi Mkito na Mdundo wanatusaidia na hilo ndio lengo kwa sababu asilimia kubwa tunafanya kazi tunazozipenda ila ikulipe pia. Unaweza kufika sehemu umepush na unachoomba upewe haupewi, hiyo inatokea kwa asilimia kubwa kwahiyo baada ya kulalamika ni kujiongeza.”
“Naishi kwa muziki tu,” aliongeza Wakazi.