Technology

Lenovo yainunua brand ya Motorola kutoka kwa Google

Watengenezaji wa komputa wa nchini China, Lenovo wamezinunua simu za Motorola kutoka kwa Google. Google imethibitisha kupitia website yake kuwa imeiuza Motorola kwa gharama ya dola bilioni 2.91.

motorola-logo-660

Lenovo itapewa brand ya Motorola pamoja na simu zake zikiwemo Moto X na Moto G. Kwa kuongeza, itapewa zaidi ya haki miliki za teknolojia 2,000 huku Google ikiendelea kusimamia haki miliki nyingi ilizozipata baada ya kuinunua Motorola miaka kadhaa iliyopita.

Motorola_RAZR_V3i_02

Dili hiyo inaipa Lenovo, yenye biashara ya smartphone iliyofanikiwa nchini China, brand inayofahamika kimataifa.

Hata hivyo Google ndio iliyopata hasara kwenye biashara hiyo kwakuwa mwaka 2011, iliinununua kampuni ya Motorola Mobility kwa dola bilioni 12.5.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents