Promotion
Kutana na Jay Ree: Mtangazaji wa msimu mpya ‘The Chart’ ya Times FM
Kipindi cha The Chart cha Times FM ya Dar es Salaam, kinachocheza nyimbo 20 bora kila Jumamosi kuanzia saa 4 kamili asubuhi hadi saa 6 mchana kimeanza msimu mpya na mtangazaji mpya, Julian Ishungisa aka Jay Ree.
Jay Ree ambaye ameshafanya show hiyo tangu mwezi uliopita amekuwa akifanya vizuri kila wiki akiwa na habari kali na mahojiano ya wasanii wakubwa duniani kote juu ya nyimbo kubwa zinazofanya vizuri.
Kabla ya kujiunga na Times FM, Jay Ree alikuwa akifanya kazi kwenye kituo cha redio cha Ebony FM cha Iringa.