Burudani
Makomando kuja na ‘Sasanuvo’
Makomando wanatarajia kuachia wimbo wao mpya ‘Sasanuvo’ pamoja na Video yake. Wimbo huo umetayarishwa na Jobanjo.
Akizungumza na Bongo5 leo, member wa kundi hilo, Muki amesema kwa sasa wananataka kuwapa mashabiki wao ladha ya muziki wanaoupenda kutoka kwao.
“Sasa hivi tunataka kuwapa mashabiki wetu muziki ambao wataufurahia na tayari pia tumeshafanya video na Kwetu Studio. Ni wimbo ambao una dance ya kuvutia na kama kawaida yetu katika kudance huwa hatubahatishi.”
Wamesema wimbo huo utatoka wiki ijayo.