Michezo

Kun Aguero na Fernandinho washushiwa rungu zito na FA

Chama cha soka nchini Uingereza FA kimemuadhibu kwa kumfungia mchezaji wa klabu ya Manchester City, Kun Aguero mechi nne baada ya kumchezea rafu beki David Luiz wa Chelsea Jumamosi iliyopita wakati timu hizo zilipokutana kwenye mchezo wa ligi kuu.

3affe97400000578-3997714-image-m-166_1480799100610

Wakati huo huo chama hicho kimemuadhibu kiungo Fernandinho kutocheza mechi tatu baada ya kumkaba kooni na kumsukuma hadi chini kiungo Cesc Fabregas.

3afe732d00000578-3997714-image-a-168_1480799119907
Fernandinho alivyo kuwa amemkaba Fabregas

Kwenye mechi hiyo Chelsea ilifanikiwa kuifunga Man City mabao 3-1 na kuendelea kuongoza kwenye msimamo wa ligi kuu ikiwa na jumla ya pointi 34 wakifuatiwa na Arsenal yenye pointi 31 huku Man City wakishuka hadi kwenye nafasi ya nne wakiwa na jumla ya pointi 30.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents