Burudani
Kumbukumbu ya Mangwea: TID asema muziki ndio kitu ambacho kilimuunganisha na Mangwea
Msanii wa muziki ambaye alikuwa rafiki wa karibu wa marehemu Albert Mangwea, TID ‘Mnyama’ katika show ya kumbukumbu ya kifo cha rafiki yake iliyofanyia Jumapili hii, amezungumzia kitu ambacho kiwaongonanisha na kufanya urafiki wao kuwa wenye nguvu mpaka mmoja wao walivyochukuliwa na Mungu.
Akiongea na Bongo5, TID amesema muziki ndio kitu ambacho kilikiwafanya wakawa marafiki wa kudumu.
“Mimi na Mangwea tulikuwa ni ndugu kabisa baada ya kuunganishwa na muziki, tulikula pamoja, tulilala pamoja. Kwa hiyo sio rafiki tu, ni ndugu kabisa,”alisema TID.