Burudani

Kumbe Dogo Janja ndiye amemrudisha Madee kurap kwenye Hela!

Unashangaa kusikia kuwa Dogo Janja ndio amemrudisha Madee kwenye kuchana? Ni muda mrefu tumekuwa tukimsikia Madee akiwa anaimba kwenye nyimbo zake kabla ya kuachia ‘Hela’ hivi karibuni.

Akiongea katika kipindi cha Flavour Express cha Maisha FM ya Dodoma na mtangazaji Silver Touchez, rapper huyo amedai kuwa alimshauri Madee arudi kwenye kurap kwa kuwa anamkubali zaidi akifanya hivyo kuliko anapoimba.

“Madee hapa katikati kawapeleka sana watu mchaka mchaka ukiangalia ‘Tema Mate’, ‘Migulu Pande’, ‘Pombe Yangu’ nikamwambia mzee rudi kidogo kwenye kurap. Mimi nampenda Mdee wa kurap sana kwa sababu anamaneno fulani ya mtaani. Kw hiyo mshua akapiga dude la ‘Hela’,” amesema Dogo Janja.

Janjaro ameongeza kwa kutaja kitu ambacho akipendi kwenye muziki, “Mimi sipendi kushindanisha nyimbo zangu mimi kama mimi. Mfano nyimbo yangu ikianza kutoka kwenye Top 10 nianze kuwa na stress kiasi kwamba nipiganie kuingiza mkwaju mwengine, kitu ambacho sikiwezi kabisa. Huwa napenda kuzipa nafasi nyimbo zangu, sipendi kuwa na muziki wa Big G yaani naachia leo baada ya miezi miwili au mitatu naachia tena, no. Napenda kuwa kwenye challenge fulani kafanya ngoma kali na mimi nafanyaje ili kuweza kufanya zaidi ya pale.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents