Burudani
Kisa cha Beyonce na Jay Z kususia harusi ya Kimye chabainika, Kimye ni tishio kwa ‘brand’ yao
Kitendo cha Beyonce na Jay Z kutohudhuria harusi ya Kanye West na Kim Kardashian kiliwashtua wengi kutokana na ukaribu wao.
Na sasa ripoti mpya zinadai kuwa Beyonce na Jay Z waliamua kuitosa harusi hiyo kwakuwa Queen Bey hakutaka kufunikwa na bibi harusi, Kim. Chanzo cha karibu kimeiambia safu ya Page Six ya gazeti la New York Post kuwa wanandao hao waliichukulia harusi ya Kimye kuwa si ya hadhi yao.
“Beyoncé hakutaka kuruhusu Kardashian amemzidi umaarufu. Na Jay hakutaka uwepo Kanye na Kim – anadhani ni mbaya kwa biashara. Nadhani Jay amepoteza heshima Kanye hapo.”