Kipre Tchetche arudi Oman kupigania uhamisho wake kutoka Azam FC
Mchezaji Kipre Herman Tchetche amerejea Oman ilikukamilisha uhamisho wa kuanza kuichezea klabu yake mpya, Al-Nahda Al-Buraimi kutoka Azam FC ya Tanzania.
Kipre Herman Tchetche alipo jiunga na klabu yake mpya, Al-Nahda Al-Buraimi
Tchetche alilazimika kurejea kwao, Ivory Coast mapema mwezi huu baada ya Azam FC kugoma kumruhusu kujiunga na Al Nahda bila dola za Kimarekani 50,000.
Na Azam ilifanya hivyo kwa sababu Tchetche aliondoka Dar es Salaam akiwa amebakiza Mkataba wa mwaka mmoja baada ya kuichezea klabu hiyo tangu mwaka 2010.
Akizungumza na binzubeiry Tchetche amesema anatarajia kumalizana na Azam FC ndani ya muda mfupi tangu sasa. “Tayari nimerudi Oman na ninatarajia kumalizana na Azam muda si mrefu ili nianze kucheza hapa,” alisema Tchetche.