BurudaniDiamond PlatnumzWema Sepetu

King Majuto ajipanga kufanya filamu ya pamoja na Wema na Diamond

Msanii mkongwe wa filamu za vichekesho nchini, King Majuto amesema hivi kariburi alimshawishi Wema Sepetu azungumze na mpenzi wake Diamond Platnumz ili wafanye kazi ya pamoja.

10508029_840308722676521_383474538_n
Diamond na Mzee Mjuto

Mzee Majuto ambaye ni mshindi wa Tuzo za Watu 2014 ya filamu inayopenda, ameiambia Bongo5 kuwa amemwachia kazi hiyo Wema ili azungumzee na mzee (Diamond).

“Hivi karibuni nilikuwa na Wema, nimemwambia aongee na Diamond ili tufanye filamu ya pamoja,” amesema Majuto. “Mimi, Wema na Diamond, hata Diamond ninaweza kuzungumza naye sema nimeanza na Wema kwanza, akikubali mtasikia tu.”

Kwa upande mwingine Majuto amesema ili acheze filamu anahitaji kulipwa shilingi milioni 3.

“Umri unaenda sasa biashara za nisaidie nisaide hakuna, kama unanitaka ili tufanye kazi unatakiwa uandae milioni 3.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents