Burudani
Kim Kardashian awachanganya mashabiki kwa picha zake mpya
Kim Kardashian ameibuka tena na picha za utata akiwa kwenye mapumziko ya muda (Vacation) nchini Mexico.
Ni muda kidogo mashabiki hawajafanikiwa kuziona picha zinazoonyesha mwili wa mke wa rapper Kanye West lakini sasa zimewafikia baada ya picha mpya za mrembo huyo kuonekana akiwa kwenye eneo la Casa Aramara Estate akicheza tennis na rafiki yake, Jasmine Sanders.
Ni takribani wiki moja sasa Kim yupo nchini Mexico huku akiendelea kupost picha za utatani. Kumbuka kuwa mrembo huyo ni mmoja kati ya mabingwa wa kupiga picha zinazowaonyesha miili yao. Tazama picha nyingine hapa chini za Kim alizopiga akiwa nchini Mexico.