Bongo Movie

Kijana anayedaiwa kutoka kimapenzi na Wema Sepetu afunguka, adai hamjui Idris Sultan

Model anayedaiwa kutoka kimapenzi na malkia wa filamu Wema Sepetu, Calisah amefunguka na kuzungumzia tetesi hizo ambazo zimekuwa zikisambaa katika mitandao ya kijamii.
wema-sepetu

Kijana huyo ambaye tayari ameshaonekana mara kadhaa katika baadhi ya video za mastaa wa muziki nchini, amemmwagia sifa malkia huyo wa filamu huku akishindwa kuweka wazi kama ni kweli anatoka naye kimapenzi au la!.

“Wema is a beautiful girl, sexy and every man’s dream, na mimi pia ni mvulana mzuri ambaye mwanamke yeyote angependa kuwa na mimi, akiwemo Wema mwenyewe,” Calisah alikiambia kipindi cha Enewz cha EATV. “Siwezi kusema moja kwa moja kwamba sisi ni wapenzi, lakini lakizima ujue kuwa Wema ni mzuri na mimi mzuri,”

Pia kijana huyo alidai kuwa hamtambui Idris Sultan na hakumbuki kama Tanzania imewahi kuwakilishwa na mtu anayeitwa Idriss katika mashindano ya Big Brother Afrika.

“Who? Idriss, kwani amewahi kuwa Big Brother? Which year?,” aliuliza kijana huyo.

Malkia huyo wa filamu toka aachane na mshindi huyo wa Big Brother Afrika 2014, hajaweka wazi mahusiano yake mapya.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents