Burudani
Kesi ya Chid Benz yasogezwa mbele mpaka December 1
Kesi inayomkabili rapper Chid Benz ya kukamatwa na madawa ya kulevya iliyokuwa ikisikilizwa leo (Nov. 11) katika mahakama ya mkazi Kisutu imesogezwa mbele hadi December 1.
Upande wa mashitaka ukiongozwa na mawakili wawili Ofmed Mtenga na Leonard Challo mbele ya Hakimu Waliarwanda Lema, umesema upelelezi bado haujakamilika nakutaja tarehe ya kusikilizwa kesi hiyo Desemba mosi.
Chid Benz yupo nje kwa dhamana kufuatiwa kukamatwa kwa madawa ya kulevya katika uwanja wa ndege Dar es salaam October 10, 2014
Source:XXL, Clouds Fm