Burudani
Kanye West aichelewesha ndege kuondoka, agoma kuomba radhi!
Kanye West ndiye aliyesababisha ndege iliyokuwa inatoka Paris kwenda Helskini kuchelewa kuondoka.
Supastaa huyo alikuwa anasafiri kutoka Paris, Ufaransa kwenda Helsinki, Finland jana asubuhi na pamoja na kupanda kwenye ndege hiyo kwa kuchelewa aligoma kuomba radhi kwa kuwachomesha mahindi abiria wengine.
Rapper huyo alipoingia ndani ya ndege hiyo na kukaa kwenye siti alikataa pia kupigwa picha na wanandoa wa Ulaya waliokuwa humo.
Chanzo kimoja kimeliambia gazeti la New York Post kuwa Kanye alikuwa akiongea kwa ishara bila kutoa sauti.