Burudani
Kanye asimamisha taxi kupiga picha na paparazzi aliyevaa t-shirt iliyomvutia, t-shirt zanunuliwa kama njugu
Kanye West hana urafiki na paparazzi.. lakini paparazzi mmoja amemvutia rapper huyo.
Kanye West akiwa na paparazzi ambaye rapper huyo aliyependa t-shirt yake
Akiwa kwenye mitaa ya jiji la New York, Alhamis wiki hii ndani ya taxi, Yeezy aliamua kusimama na kushuka kumpiga picha paparazzi aliyekuwa akimpiga picha kwakuwa alipenda tu t-shirt aliyokuwa amevaa.
Kanye: T-shirt kali sana hiyo dogo, umenunua wapi?
Kanye pia alipiga picha kadhaa na paparazzi huyo sharobaro. Matokeo ya tukio hilo ni kwamba kampuni inayotengeneza t-shirt hizo imeneemeka baada ya mauzo kuongezeka ghafla.
Kampuni hiyo iitwayo D9 Reserve iliuza zaidi ya t-shirt 300 ambapo kila moja ni dola $135 ndani ya saa chache tangu Kanye afanye uchawi wake!