Habari
Kampuni ya ndege ya Korea kusitisha safari zake za Kenya kwa hofu ya Ebola
Kampuni ya ndege ya Korea imesema itasitisha safari za ndege zake kwenda nchini Kenya kuanzia Agosti 20 Kufuatia hofu ya kuenea kwa ugonjwa wa Ebola.
Korean Air Lines Co Ltd imesema kuwa ndege zake zimekuwa zikifanya safari mara tatu kwa wiki kutoka Incheon, Korea Kusini kwenda Nairobi.
Hatua hiyo imekuja baada ya shirika la afya duniani kutahadharisha kuwa Kenya inaweza kuwa katika hatari ya kukumbwa na ugonjwa wa Ebola kutokana na kasi ya kuenea kwa ugonjwa huo.
Hatari hii inatokana na Kenya kuwa kitovu cha usafiri wa ndege huku wasafiri wengi wanaokwenda Afrika Magharibi wakipitia nchini humo.
Source: Reuters/BBC Swahili