Burudani
Kadja wa ‘Maumivu’ aahidi kuonesha uwezo wake wa kuimba mbele ya Sauti Sol
Msanii anayefanya vizuri na wimbo ‘Maumivu’ Kadja Nito kutoka THT amesema atahakikisha anaonesha uwezo wake wote wakati atakapokuwa akitumbuiza kwenye jukwaa moja na kundi la Sauti Sol la Kenya.
“Mashabiki wangu wakae tayari kwa kazi yangu mpya na na pia nafurahi kupata nafasi ya kufanya show na wasanii wakubwa kutoka Kenya Sauti Sol jukwaa moja. Ni nafasi nzuri kwangu kwa kuonesha uwezo wangu wa kuimba live na bendi pale Escape 1 August 30 katika show ya Beauty and Music Night,” amesema.
Wasanii wengine watakaotumbuiza ni pamoja na Yamoto Band na Mirror.