Burudani
Juu ya Vanessa na Jux yaingia kwenye playlist ya The Beat London FM ya UK
Wimbo wa Vanessa Mdee na Jux ‘Juu’ umeingia kwenye playlist ya kituo cha redio cha The Beat London FM ya Uingereza.
Baada ya taarifa hiyo kupitia mtandao wa Instagram, Vanessa Mdee ambaye yupo nchini Marekani kwa ajili ya tamasha la One Africa Music, ameandika, “Mad love to ALL THE DJs AROUND THE WORLD bumping #Juu ???? Asante Sana. Na bado tunaenda Juu baby. #London is switched on.”
Kwa sasa imeonekana ni hatua kubwa muziki wa Bongo Fleva umepiga kwa kuanza kupata tobo lake ikiwa ni mwezi mmoja umepita tangu kituo cha redio cha BBC Radio 1Xtra kuutangaza wimbo wa ‘Kidogo’ wa Diamond kuingia kwenye playlist ya kituo hicho.