Burudani

Juma Nature asema hana mpango wa kutoa album wala kushoot video nje ya nchi

Juma Nature amedai kuwa hafikirii kwenda kushoot video zake nje ya nchi kama wasanii wengi wa Tanzania wanavyofanya. Nature amesema anaamini kuwa hapa nchini kila kitu kinawezekana.

Juma Nature

“Mie video zangu zote nitafanyia hapa hapa labda nikienda huko Ulaya kufanya show ndo nitaweza kufanya video lakini eti natoka hapa sijui naenda kufanya huko video siwezi,” amesema Nature. “Hapa Tanzania nina uhakika kuna vijana wengi sana wamesomea mambo ya production nawapo vizuri inabidi tuwatumie hawa vijana na bongo. Kuna malocation ya ukweli inatakiwa sisi ndo tutangaze nchi yetu na tamaduni zetu kwa kufanya video hapa nyumbani. Lakini sisi tukienda kufanya video huko nchi za watu tutakuwa tunawatangazia wao nchi zao, kwahiyo lazima tuwe wazalendo na nchi yetu.”

Katika hatua nyingine, Nature amesema ni ngumu kutoa album tena kwa sasa kwakuwa teknolojia imeharibu mfumo uliokuwa ukiwezesha kuuzwa kwa album na msanii akapata faida.

“Unajua sasa hivi pamekuwa na technology sana tofauti na zamani. Sasa hivi hata ukisema unatoa album haitafanya vizuri kama zamani. Na hii Tanzania yetu ndo kabisaa atanunua mmoja halafu ataweka kwenye mtandao wengine wataanza kudownload utajikuta hujafaidika na chochote inabidi serikali itusaidie hilo suala,” amesema.

Kuhusu mikakati ya kundi lake la TMK Halisi, Juma Nature amesema: Tupo na tunafanya kazi muda si mrefu tutatoa kazi mpya zinakuja. Tulikuwa tunarekodi mangoma ya ukweli, najua Bongo5 mtakuwa wa kwanza kupata hiyo midundo. TMK Halisi ipo na watu wapo wanapiga mzigo wala haijafa tena tupo vizuri sana.”

Juma Nature

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents