Burudani
Jua Cali apanga kumshirikisha Joh Makini
Rapper kutoka nchini Kenya, Jua Cali amesema anatamani kumshirikisha Joh Makini kwenye album yake mpya iitwayo Mali ya Umma inayotarajiwa kutoka October waka huu.
Akizungumza na 255 ya XXL kupitia Clouds FM, Jua Cali alisema akimpata Joh Makini na akashirikiana naye atafurahi.
“Album itatoka October, September,” alisema. “Jina la album inaitwa Mali ya Umma (Public Properties). Najaribu kumtafuta Joh Makini, huyo ndio nataka kufanya naye kazi yuko sawa kabisa, so nikimpata nitashukuru sana,” alisisitiza rapper huyo.
Jua Cali alifahamika zaidi nchini kwa nyimbo kama Kwaheri, Bidii Yangu na zingine.