Burudani
Joti kuachia filamu yake ya kwanza ya komedi ‘Sanduku la Babu’
Msanii wa vichekesho wa kundi la Orijino Komedi, Joti anatarajia kuachia filamu yake ya kwanza ya vichekesho itayoangaliwa na watu wa rika zote. Filamu hiyo inaitwa Sanduku la Babu.
“Kwa mara ya kwanza Tanzania,Joti ametoka na comedy inayoitwa ‘sanduku la babu’itakayo tazamwa na rika zote,kaka, dada, watoto,wazee….kaa tayari,” Joti ameandika kwenye Instagram.
Katika filamu hiyo Joti atacheza katika uhusika mbalimbali, akiwa kama mwanamke, mzee, kijana nk.