Burudani

Johari akanusha kutaka kufunga ndoa na Ostaz Juma

Msanii wa filamu nchini, Blandina Chagula maarufu kama Johari amekanusha kuwa na uhusiano wa kimapenzi na meneja wa Mtanashati Entertainment, Ostaz Juma.
johari
Ostaz Juma na Johari

Akizungumza kwenye kipindi cha The Cruise cha East Africa Radio, Johari alisema kuwa hajawahi kuwa na uhusiano ya kimapenzi na Ostaz Juma wala Ray. “Ni kweli haya mambo yanakuwa yanatokea na kuzushwa lakini ukweli kwamba sijawahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Ray ,lakini mahusiano yetu ni ya kikazi tu,lakini pia sijawahi kuwa na uhusiano na Ostaz Juma,”alisema Johari.

Johari alifafanua kuwa uhusiano wake na Ray unatokana na wao kuwa wakurugenzi kwenye kampuni yao ya filamu, RJ Company.

“Ni kweli Ray ni mkurugenzi mwenzangu katika kampuni yetu RJ ila sina mahusiano naye kimapenzi na sijawahi kugombana na Chuchu wala msanii mwingine yoyote yule kwa sababu ya mahusiano ya mapenzi.

Kwa upande wake, Ostaz Juma alidai kuwa Johari amemkana hana cha kufanya na atachukulia poa.

“Harusi bwana ni safari ndefu sana mpaka unakuja kufunga ndoa na mtu kuna vitu vingi sana inabidi ujipange, mzungumze,muafikiane, kuna vitu vinaweza kutoea vikaharibu harusi tena,ila kama amesema hivyo poa, najua hata yeye ni mwanadamu,sasa kama yeye nafsi yake imemtuma kusema hivyo basi lakini atatambua kwamba Ostaz Juma na Musoma alikuwa anampenda.Unajua mwanamke anaweza kutembea hata na wanaume mia mbili ,lakini anaweza akakwambia nimetembea na wanaume fulani,” alisema.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents