Burudani
Jibu la Lundenga kuhusu nani atapewa taji la Miss Tanzania 2014 kama ikibainika Sitti Mtemvu alidanganya umri
Inawezekana wewe ukawa miongoni mwa wengi wanaofuatilia skendo ya Miss Tanzania 2014, Sitti Mtemvu na inawezekana pia umeshajiuliza nini kitatokea uchunguzi wa BASATA utakapokamilika na ikibainika kuwa alidanganya umri wake.
Baada ya mwenyekiti wa kamati ya Miss Tanzania bwana Hashim Lundenga kuulizwa na 255 ya XXL ya Clouds Fm, kama ‘ikitokea’ Sitti akijivua taji/akithibitika alidanya umri, taji hilo atapewa nani au shindano litarudiwa? hiki ndicho alichojibu:
“Sitaki kuzungumza hiyo sitaki kuzungumza mpaka ikitokea tutajua nini la kufanya lakini haijatokea kwamba taarifa hizi ziko sahihi”.