Burudani
Jay Z na Beyonce wakumbushia viapo vyao vya ndoa
Beyoncé na Jay Z wameamua kuzizika kabisa tetesi za kuwa ndoa yao imekufa kwa kukumbushia viapo vyao vya ndoa.. ama kwa lugha rahisi kufunga ndoa tena.
Kwa mujibu wa jarida la People, mastaa hao waliosherehekea miaka sita ya ndoa yao mwezi April, hivi karibuni walifunga ndoa tena.
“Walikuwa na matatizo makubwa,” chanzo kimoja kimeliambia jarida hilo.. “Lakini walimaliza na kuamua kufunga ndoa tena.”