Burudani
Jay Sean ajiondoa Cash Money Records
Jay Sean ametangaza kujiondoa kwenye label ya Cash Money Records.
Hata hivyo, Sean amesema hana tatizo na timu ya Cash Money. “Bado nina uhusiano mzuri na Slim na Baby [CEOs wa Cash Money],” ameuambia mtandao wa Billboard.
“Waliamini katika kipaji changu na ushirikiano wetu ulileta mafanikio makubwa,” alisema.
Hata hivyo msanii huyo alidai kuwa alitaka kupata kitu kingine.