Burudani
Jay Moe amtaja Solo Thang kama mwalimu wake wa rap ya Kiswahili
Jay Moe amemtaja Solo Thang kama rapper muhimu kwenye career yake.
Amedai kuwa rapper huyo ndiye aliyemsaidia kuweza kuandika mashairi ya rap ya Kiswahili.
“Solo Thang ni mtu ambaye nilikuwa naye karibu sana. Kipindi kile alikuwa ananisaidia sana kwenye uandishi wa kiswahili,” alisema.
“Unajua wakati ule tulikuwa tumejiunga kuwa Wateule wengine tulikuwa tunaenda tunashinda pale tulikuwa tunarap sana Kiingereza. Solo yeye alikuwa mtaalam sana wa Kiswahili ndio akawa ananielekeza.”