Burudani

Jah Prayzah azidi kunogewa na Bongo Flava

Ni dhahiri, Jah Prayzah amenogewa na ladha ya muziki wa Bongo Fleva.

Muimbaji huyo kutoka Zimbabwe, anamshukuru Diamond kila kukicha, ambaye alimshirikisha katika wimbo wake wa ‘Wotora Mari’ na kumpatia tobo kubwa Afrika kwa kuanza kusikilizwa zaidi maeneo mbalimbali Afrika, na kupelekea kujinyakulia tuzo ya Listener’s Choice Awards ya MTV MAMA mwaka jana.

Sasa mkali huyo ameonekana akiwa studio na msanii kutoka WCB, Harmonize na kuandika ujumbe katika mtandao wa Instagram unaoashiria maandalizi ya wimbo wao mpya.

“In the studio again with another Tanzanian big star @harmonize_tz .Zimbabwe neTanzania ?,” ameandika Jah katika mtandao huo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents