Bongo Movie

Jaguar kutua TZ kwajili ya Uwoya, Irene adai anakuja kufanya mipango ya ndoa yao

Msanii wa muziki kutoka Kenya, Jaguar ameweka wazi hisia zake za kumkubali sana staa wa filamu Irene Uwoya kutoka Bongo, ambapo amesema anajipanga kutua Bongo mwishoni mwa mwaka huu kuja kumuona staa huyu anayevutiwa naye.

jaguar-pic
Jaguar

Jaguar ameiambia E-Newz ya Eatv kuwa akitua Bongo hataishia kumuona Irene tu, bali atakwenda hadi kwa wazazi wa staa huyu kwa lengo ambalo hajalifafanua zaidi.

“Mimi naona nitue Tanzania, sijui nije December, sijui nimuijie Irene Uwoya, nije kumchukua, mwambie naja kumchukua, ameniambia nione wazazi kwanza, naja December kumchukua,” alisema Jaguar.

irene-uwoya
Irene Uwoya

Baada ya kauli hiyo Bongo5 ilimtafuta Uwoya na kuzungumzia ujio huo wa Jaguar ambao amesema anaufahamu, na akadai anakuja kufanya mipango ya kumuoa.

“Tunampango wa kuoana, bado anakuja,” alisema Irene Uwoya huku alifurahi.

Msikilize hapa Irene

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents