Burudani

Izzo Bizness ataja gharama aliyotumia kufanya video ‘Walalahoi’

Rapper kutoka Mbeya, Izzo Bizness, amesema video ya wimbo wake ‘Walalahoi’ imetumia kiasi cha shilingi milioni 1 na laki 4 peke yake.

Izzo
Akizungumza na Enewz ya EATV, Izzo amesema video imechelewa kukamalika kwa sababu muongozaji wake amekuwa na kazi zingine nyingi wakati huu.

“Kuna vipande vichache tu vimebaki kwa sababu nyimbo yenyewe unaiona ilivyo, tumeongea mambo mengi, na sio muda ambao unahitaji kushoot unashoot tu. Unaweza ukahitaji kushoot director ana kazi nyingine tatu, nne kwahiyo unasogezwa mbele. Ndio maana imechelewa. Pia watu wategemee video kali kabisa. Video ni milioni 1 na laki 4 na Nick hapo tumemlipa kila kitu,” alisema Izzo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents