It’s a baby girl: Zari na Diamond wapata mtoto wa kike
Diamond Platnumz na Zari the Bosslady wamepata mtoto wa kike, Latiffah Naseeb Abdul aka Tiffah Dangote.
Mama Diamond akiwa amembeba mjukuu wake, Latiffah pembeni ya mama mtoto, Zari
Mtoto huyo ameingia duniani saa 10 na dakika 40 Alfajir, Alhamis hii.
04:40am 06 August 2015
— Diamond Platnumz (@diamondplatnumz) August 6, 2015
Haijaweza kufahamika kwa mara moja ni hospitali gani mtoto huyo amezaliwa kwa kile meneja alichosema ‘usalama wa mama na mtoto’ kwakuwa bado wapo hospitali.
“Sura ya mama yangu inatosha kueleza ni kiasi gani najiskia ndani ya Moyo wangu, karibu kwenye ulimwengu @princess_tiffah,” ameandika Diamond kwenye picha hiyo juu aliyoiweka Instagram.
Awali Diamond alisema kuwa Zari angejifungulia Tanzania.
Moja ya kabati ya nguo za Latiffah
Tayari mtoto huyo amefunguliwa account ya Instagram iitwayo princess_tiffah.
“Welcome to the Next Most Famous Daughter in Africa… My dad and Mom decided to call me Latiffah but I wanna be called Latty or Tiffah, #Princesstiffa #Lattyplatnumz,” yanasema maneno kwenye picha ya kwanza kwenye akaunti hiyo.
Tunawapongeza mastaa hao.