Burudani
IK na Minnie Dlamini kuhost tuzo za AMVCAs
Africa Magic na MultiChoice wamewatangaza washereheshaji wawili wa tuzo za mwaka huu za Africa Magic Viewers’ Choice [Awards] (AMVCAs).
Washereheshaji hao ni mrembo wa Afrika Kusini, Minnie Dlamini pamoja na host maarufu wa BBA, IK Osakioduwa wa Nigeria.
Tuzo hizo za nne kufanyika zitatolewa March 5. Vipengele 26 vinashindaniwa. Lulu ni miongoni mwa waigizaji waliotajwa kuwania tuzo hizo zitakazotolewa jijini Lagos, Nigeria.