Burudani
Iggy Azalea atangaza jina la album yake mpya
Hit maker wa ‘Fancy’, Iggy Azalea yuko kwenye foleni ya wasanii wanaotarajia kuachia album zao mpya hivi karibuni, na tayari ametangaza album yake itaitwa ‘Digital Distortion’.
Rapper huyo wa Australia ametoa taarifa kuhusu album yake Oct.6 kupitia Twitter alipokuwa akijibu maswali ya mashabiki wake.
Pia alisema kuwa single ya kwanza ya kwenye album hiyo itatoka mwezi huu, lakini album yenyewe itatoka mwakani 2016.
‘Digital Distortion’ itakuwa ni album pili ya star huyo kufuatia ‘The New Classic’ iliyotoka mwaka 2014 ambayo ilikuwa na hits kama ‘Fancy’ na ‘Black Widow’.