Burudani
Iggy Azalea aeleza sababu ya kumpiga chini Nick Young
Iggy Azalea ametaja sababu iliyomfanya aachane na aliyekuwa mpenzi wake, Nick young.
Mahusiano ya Iggy na Nick yaliingia dosari baada ya kuvuja kwa mazungumzo ya siri March 24 mwaka huu yaliyomhusisha Nick na mchezaji mwenzake D’Angelo Russell wakiongea kuhusu kutongoza wanawake wengine. Aidha Juni 20 Iggy alitangaza kuvunja uhusiano wake na Nick na kuondoka kwenye nyumba waliokuwa wakiishi huko Los Angeles inayomilikiwa na mpenzi wake huyo.
Huu ni ujumbe alioandika Iggy Azalea kupitia akaunti yake ya Twitter: