Burudani

Ifahamu TV1: Kituo kipya cha TV, Tanzania kinachomilikiwa na kampuni ya Sweden (MTG) kitakacholeta mapinduzi ya vipindi vya burudani

ITV, EATV, Channel Ten, Star TV na vituo vingine vya runinga Tanzania vimepata mpinzani mwenye nguvu. Ni kituo kipya kiitwacho TV1. Kituo hicho kinamilikiwa na kampuni ya Sweden iitwayo, Modern Times Group.

a5e05a3a13b7399c_400x400ar
Logo ya TV1

Kampuni hiyo iliyojikita zaidi kwenye masuala ya burudani imeanzisha kituo hicho mapema mwaka huu na kwake ikiwa ni TV ya kwanza ya bure kuwahi kuianzisha.

02e9fb3e961311e3a75b0eb115e847c3_8
Newsroom ya TV1 iliyopo Mikocheni, Dar es Salaam. Channel hiyo tayari inaonekana kupitia ving’amuzi vya Startimes na inawafikia asilimia 38 ya wananchi wa Tanzania

8b9aa358961211e3a343120758c0a81e_8

d1e3d5b894f111e3a8e40ef055ffcfaa_8
George Tyson, director wa vipindi wa TV1

TV1 itakuwa ni channel ya burudani itakayokuwa pia mchanganyiko wa habari zilizoandaliwa nyumbani na za kimataifa pamoja kurusha filamu za kimataifa na TV series.

dfdacc9094f011e3ad271296246e27d8_8
Vanessa Mdee akiwa kwenye set ya show yake ‘The One Show’ ya kituo hicho

eedaa94a94f011e3a96712b7b8d9156b_8
Vanessa Mdee akifanyiwa make-up

a0de3b7c94ef11e3adca0e50b5ae6e66_8
Vanessa Mdee

62518c0a94f011e3aaff12e553090a3f_8

TV1 ni channel ya pili ya bure ya kampuni ya MTG iliyoanzisha barani Afrika, baada ya kituo cha Viasat1 kilichopo nchini Ghana kilichoanzishwa mwaka 2008.

48459d5c958011e393a00e5d5ec921df_8
Watangazaji wa habari wa TV1, Nzowa na Agnes

Tayari kituo hicho kimeajiri watangazaji mbalimbali wazoefu kufanya vipindi mbalimbali wakiwemo Marygoreth Richard aliyekuwa msomaji wa habari za East Africa Radio, Angel Karashani (TPF6) na aliyewahi kuwa mtangazaji wa Channel Ten, Nzowa

e9dcab3e94f311e3b2f5124e8fde040d_8
Angel Karashani

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents