Michezo

Ibrahimovic kuondoka PSG mwishoni mwa msimu huu

Mshambuliaji wa klabu ya Paris St-Germain Zlatan Ibrahimovic anaondoka katika klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu.

340E2B9F00000578-3588474-image-a-1_1463128830831

Mkataba wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34 unakamilika msimu huu na amehusishwa na uhamisho wa Manchester United,kilabu ya Los Angels Galaxy na AC Milan.

”Ninafurahia”,alisema.”Niliwasili kama mfalme na sasa naondoka kama kigogo lakini ntarudi”.

PSG imesema kuwa Ibrahimovic anaondoka kama mshambuliaji bora na mchezaji bora zaidi katika historia ya kilabu hiyo.

Ibrahimovic ameifungia mabao mengi zaidi klabu hiyo licha ya kujiunga nayo mwaka 2012 aiwa amefunga mabao 152 katika mechi 178.

PSG imeshinda taji la Ligue 1 kila msimu tangu Ibrahimovic ajiunge na kilabu hiyo.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents